Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, maelezo kamili ya barua muhimu ya Ayatollah Alireza A'rafi, Mkurugenzi wa hawza na Rais wa Baraza la Siasa la Kambi ya vita ya kubainisha "Bila'gh Mubīn", ni kama ifuatavyo:
Bismillahir Rahmanir Rahim
Wanafunzi watukufu, wasomi, walimu, wanajihadi, vikundi vya jihadi, mashirika ya kidini, na kwa waheshimiwa wote, taasisi, wasimamizi, na wajumbe wa vyuo vya kidini na shughuli za ulinganishaji — salama kwao wote kwa neema ya Mwenyezi Mungu.
Nikiwa na salamu za dhati, nikiwa na heshima kubwa kwa manabii na waja wema wa Mungu, hasa kwa Mtume Muhammad (s.a.w) na Imam wa Zama (a.s), na tumkikumbuka na kumheshimu Imam Ruhollah (rah), mashahidi waliotukuka, hasa Imam Shahidi (rah), watoto, vijana na wanawake mashahidi, waheshimiwa na makamanda mashahidi, na vilevile mashahidi wa nguvu za kijeshi za Iran, napenda kutoa pongezi kwa kuikaribisha Eid al-Fitr na kuanza mwaka mpya.
Nashukuru na kuthamini michango ya kila mmoja wenu, taasisi, vikundi vya wahadhiri na mashirika ya kidini na ya Hawza, na vilevile shukran zangu ziwaelekee "Kambi ya Bala'gh Mubīn" kwa juhudi zao za kiutamaduni, ulinganiaji, huduma na jihadi waliyoitoa wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na likizo ya mwaka mpya, na hasa kwa mchango wao wa kipekee katika vita vya Ramadhani na uwepo wao wa kishujaa katika ulinganiaji na kutoa huduma kwa wananchi shujaa na vijana walio jitolea katika "Vita vya Ramadhani." Pia, kwa heshima, ninataka kusisitiza baadhi ya masuala yafuatayo:
1. Vita vya Ramadhani ni hatua mpya, ya kihistoria, na ya kimkakati katika safari ya Iran, ulimwengu wa Kiislamu, Mapinduzi ya Kiislamu, ukanda, mfumk wa muqawama, na harakati ya kidini ya Hawza na Waislamu. Haya ni mapambano makubwa, kuanzisha muktadha mpya wa ujasiri na kujitolea kwa Waislamu dhidi ya mifumo ya kifasadi. Kwa neema ya Mwenyezi Mungu, msaada wa familia ya Mtume (saww), na mwongozo wa kiongozi wetu mkuu, vita hii imejaa mafanikio makubwa.
2. Majukumu ya Hawza, Waislamu na sisi sote katika ulinganiaji na vita hii ni muhimu sana. Tukifuata maagizo ya Imam Ruhollah (rah), Imam Shahidi (rah), Kiongozi Mkuu, na Mabaraza ya Kiislamu, tunapaswa kuvifanya vita hivi kama kipaumbele, na kuhakikisha kuwa tunasaidia na kuwaelimisha wapiganaji wa Kiislamu na taasisi za kijeshi kwa kufanya kazi katika ulinganiaji na kutoa huduma. Hivyo, kila taasisi, shule na mashirika lazima watumie rasilimali zao kwa pamoja ili kuimarisha kazi ya kuelimisha.
3. Kujenga mnyororo wa shughuli za kitamaduni na kuunganisha rasilimali za ulinganishaji, leo hii ni jambo muhimu zaidi kuliko wakati mwingine wowote. Hii inahitaji ushirikiano wa taasisi na mashirika, mipango ya pamoja, na ushirikiano wa vijana wa Hawza, vikundi vya jihadi na wahadhiri wa kidini. Pia, ni muhimu kushirikiana na wanajihadi kwenye miji na jamii mitaani.
4. Kutumia mfumk wa kimataifa na kuelewa hali ya dunia ni jukumu la Hawza katika kuelezea mafundisho ya Kiislamu na Mapinduzi, ukweli wa vita, na ukubwa wa mapambano haya kwa mataifa na mashirika duniani. Tunahitaji kuelewa ukweli wa hali halisi, changamoto zinazotukabili, vita vya kiakili duniani, na kuondoa hofu kwa umma duniani.
5. Hawza na Wanazuoni wamekuwa wanajeshi jasiri katika historia yao, wakiongoza katika mapambano na kujitolea kwa watu wao. Licha ya mafanikio ya kielimu, kiroho na kimaadili, leo hii ni muhimu kuchanganya juhudi za kijamii katika vita dhidi ya wakoloni wa Kimarekani na Israeli.
Ninamwomba Mwenyezi Mungu ajaalie afya, heshima, na mafanikio kwa wote, na pia amshinde adui yeyote ambaye anajaribu kuukandamiza Uislamu na Waislamu.
Na ushindi ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu, mwenye nguvu na mwenye hekima.
Alireza A'rafi
Mkurugenzi wa Hawza na
Rais wa Baraza la Siasa la vita ya ubainifu "Bala'ghu Mubīn"
Maoni yako